• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

Imewekwa tarehe: July 3rd, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MAZINGIRA bora ya biashara yanayochochewa na mahusiano mema ya Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, yanaendelea kukuza biashara, mitaji na uwekezaji, hivyo kuzalisha faida inayorejeshwa kwa umma.

Kampuni ya Saruji Tanga, ni miongoni mwa taasisi zinazonufaika kwa mazingira bora hayo, hivyo kushawishika kuunga mkono jitihada za kuwawezesha wanawake na vijana mkoani Tanga.

Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Hakan Gordal, leo Julai 3, 2025, amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, bajaji 10 za kisasa zinazotumia umeme badala ya mafuta, zenye thamani ya jumla ya Shilingi milioni milioni 65.

Amesema bajaji za umeme ni sehemu ya uthibitisho wa utekelezaji wa sera za kampuni katika utunzani mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi yanayochangiwa na uchafuzi wa hewa.

Gordal, hatua ya kutoa bajaji hizo inazotokana na mawasiliano yao na Mhe Balozi Dkt Batilda, aliyeainisha mahitaji ya vyombo vya usafiri wa kibiashara hususani kwa wanawake na vijana wa makundi maalum.

Amesema Tanga ni eneo la kimkakati kwa biashara yao inayotarajiwa kuzalisha saruji itakayouzwa nje ya nchi katika siku chache zijazo.

Kwa mujibu wa  Goldal, ufanisi na mafanikio ya kampuni hiyo vinachangiwa kwa kiasi kikubwa na mahusiano mema kati yao (wawekezaji), Serikali na wakazi wa mkoa wa Tanga kunapofanyika shughuli za uzalishaji wa saruji.

Naye Mhe Balozi Dkt Batilda, amesema imekuwa ’safari ndefu’ ya mazungumzo na uongozi wa kampuni hiyo, hasa baada ya kuwepo hisia za kufungwa kwa uzalishaji, kutokana na kununuliwa na kampuni ya Saruji Twiga.

Amesema, ushuhuda uliopo Tanga unathibitisha kuwepo wawekezaji walionunua viwanda vya awali, kutoviendeleza na wengine kung’oa mitando na kuihamishia mikoa kama vile Arusha na Dar es Salaam.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, kwa hali hiyo, kampuni ya Saruji Tanga inakuwa miongoni mwa wadau wakubwa wanaotekeleza dhamira ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuurejesha mkoa huo kuwa wa viwanda.

Amesema uzalishaji na biashara ya kiwanda hicho, utaendeleza ukuzaji wa pato la mkoa huo na Taifa, huku kukiwa na ustawishaji wa maisha ya watu kupitia ajira zilizo na zisizokuwa za moja kwa moja.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, miongoni mwa wanufaika wa awali wa bajaji hizo ni wasichana watatu wanaoendesha bodaboda na wanaoishi na ulemavu wawili.

Amesema wanufaika hao na wengine, wataingia mkataba wa marejesho utakaowezesha kupata fedha za kuagiza bajaji nyingine ili kuongeza idadi ya wanufaika.

 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.