• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

DK ABBAS: MAAFISA MAWASILIANO NA HABARI WA SERIKALI MSHIRIKI KUYAKABILI MAJANGA

Imewekwa tarehe: April 10th, 2025


 

Na Mashaka Mgeta, MOROGORO

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk Hassan Abbas, amewataka Maafisa Mawasiliano na Habari wa Serikali, kuweka na kutumia mikakati ya mawasiliano kutoa taarifa sahihi na kushughulikia matukio yanayohusiana na majanga yanayotokea kwenye maeneo yao.

Dk Abbas alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali kati ya Agosti 11, 2017 hadi Januari 31, 2020 alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Februari 14, 2023 alihamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii akiwa katika wadhifa huo hadi sasa.

Ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) ulioanza Aprili 8 na kufikia ukomo wake Aprili 12, 2025 mjini Morogoro.

Dk Abass amesema yapo mambo yanayotarajiwa na yasiyotarajiwa kutokea kwenye taasisi za umma, yakiwa ni dharura ama majanga, hivyo ni jukumu la Maafisa hao kuyabaini mapema na kuushauri uongozi namna bora ya kukabiliana nayo.

Amesema, majanga yanapotokea yanawagusa Maafisa Mawasiliano na Habari wa Serikali, hivyo kuwajibika kwa kuwa na mkakati wa kuyakabili, kutoa taarifa sahihi na kulinda hadhi ya taasisi zao.

Kwa mujibu wa Dk Abbas, utoaji taarifa sahihi wakati wa majanga unachangia kujenga imani kwa umma, kwamba taasisi husika inatambua, kushughulikia na kuepusha upotofu kuhusu janga husika.

Naye Mwenyekiti wa TAGCO, Karimu Meshack amesema Maafisa Mawasiliano na Habari wanapaswa kutambua uhusika wao wakati wa majanga na kuepuka kasumba ya kujiweka kando kwa visingizio kama vile ‘kutoshirikishwa’,

Naye Mtafiti na Mtaaluma wa Mkakati wa Mawasiliano wa Chuo Kikuu cha dar es Salaam, Dk Sophia Ndibalema amesema kukaa kimya wakati wa majanga, kunatoa mwanya wa wasiokuwa na dhamana, kutoa taarifa zinazoweza kuibua taharuki ama kuipotosha jamii.

Mwisho

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.