• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

DK KIJAJI ATOA SALAAM ZA RAIS SAMIA MIRADI YA NGUVU ZA WANANCHI

Imewekwa tarehe: January 11th, 2025

Na Mashaka Mgeta, HANDENI

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Mhe Dk Ashatu Kijaji, amezielekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) kukamilisha miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi, ili kufikia azma ya kujitegemea kwa maendeleo na ustawi wao.

Mhe Dk Kijaji amesema kukamilishwa kwa miradi hiyo ni miongoni mwa vipaumbele na maagizo ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa viongozi wa wilaya, halmashauri za wilaya, miji, manispaa na majiji zilizo katika ngazi za msingi kwenye jamii, kunapobuniwa, kuibuliwa na kuanzishwa miradi hiyo.

Ameyasema jana Januari 10,2025 katika kijiji cha Kwedikwazu Mashariki wilayani Handeni, kufuatia rai iliyowasilishwa na wakazi wa kijiji hicho wakitaka zahanati iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi mwaka 2013, na kutengewa fedha na halmashauri ya wilaya ya wilaya ya Handeni, ikamilike ifikapo Januari 30, mwaka huu kama ilivyoelezwa na waziri huyo.

Mhe Dk Kijaji anayehitimisha ziara yake ya siku tano mkoani Tanga leo, amesema agizo na nia ya Mhe Rais Dk Samia kuhusu miradi inayoanzishwa kwa nguvu za wananchi ni kukamilisha kwake, hivyo kama ikishindikana kufikia hatua hiyo, inakuwa ni ‘mzigo’ unaopaswa kubebwa na viongozi wa LGAs kwenye maeneo husika.

‘’Mhe DC (Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe Albert Msando), kama zahanati hii haitakamilika ifikapo Januari 30, 2025, hili halitakuwa jambo la Mhe Rais Dk Samia ambaye Septemba 4, 2024, alileta Shilingi milioni 50 kupitia halmashauri ya wilaya Handeni ili kumalizia ujenzi huu…litakuwa jambo lako,’’ amesema.

Hata hivyo, Mhe Msando amesema, usimamizi wa ujenzi wa zanahati hiyo umefanyika kwa vipindi tofauti kupitia ofisi yake, na kwamba uhakika wa kukamilika kabla ama tarehe 30 Januari, 2025 ni wa uhakika.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Saitoti Stephen, amesema kukamilisha kwa zahanati hiyo kutawapunguzia wakazi wa Kwedikwazu Mashariki kadhia ya kufuata huduma za afya kwenye kituo cha afya Kabuku, umbali wa takribani kilomita tano.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

    June 18, 2025
  • RAS TANGA 'AWASHUKIA' WATUMISHI WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI

    June 18, 2025
  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.