• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

HALI YA HEWA, MADENI VIKWAZO UKUSANYAJI MAPATO TANGA

Imewekwa tarehe: March 7th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

ATHARI zinazotokana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuwepo kwa wadaiwa sugu, vimebainika kuathiri ukusanyaji mapato wa Mamlaka za Serikali za Mitaa mkoani Tanga.

Taarifa ya Sekretarieti ya Mkoa (RS) iliyosomwa na Mkuu wa Idara ya Mipango, Amina Said kwenye Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) Machi 6, 2025, imeeleza, kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2024, mvua kubwa iliyonyesha wilayani Muheza, ilipukutisha maua ya machungwa, zao linalochangia takribani asilimia 30 ya mapato yake.

Hali hiyo ilisababisha kushuka kwa uzalishaji, na makusanyo yakawa Shilingi 1,198,907,161 badala ya Shilingi 3,280,710,000, ikiwa ni asilimia 37 kati ya 50 zilizokusudiwa.

Wakati mvua nyingi zikinyesha Muheza, wilaya ya Kilindi ilikabiliwa na ukame kiasi cha kupunguza uzalishaji wa mahindi na maharage yaliyo chanzo kikuu cha mapato yake.

Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ilipangiwa kukusanya Shilingi 3,561,693,000, lakini ikakusanya Shilingi 1,500,132,385, sawa na asilimia 42 kati ya 50 iliyokusudiwa.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, halmashauri ya wilaya Pangani kwa kipindi cha Julai hadi Desemba, 2024, ilikusanya chini ya malengo yake, kutokana na hali ya hewa ya baharini, ikiwemo upepo mkali ulioathiri uvuvi na ushuru unaotokana na mazao ya baharini.

Nayo halmashauri ya Jiji la Tanga iliyopangiwa Shilingi 21,060,272,000, ilifikia Shilingi 9,715,657,801 sawa na asilimia 46 kati ya 50 zilizotarajiwa.

Sababu ya kushindwa kufikia lengo ni kutolipwa ushuru wa madini yanayotokana na madini ya Iimestone na vifusi kutoka viwanda vya saruji.

Kwa hali hiyo, mapato ya mkoa wa Tanga kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 31, 2024, yalifikia Shilingi 23,053,472,275 sawa na asilimia 48 ya malengo ya Shilingi 47,554,027,000.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA ARIDHISHWA NA WANAWAKE KUSAIDIANA, KUSEMEANA MAZURI

    May 12, 2025
  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.