• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

JAJI MKUU AMKABIDHI RC MALIMA MWONGOZO KUREKEBISHA DOSARI, UTENDAJI WA MAHAKAMA TANGA

Imewekwa tarehe: May 19th, 2022

NA ESTHER MBUSI, OMT

Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima fomu ya mwongozo inayomtaka mwananchi yeyote ambaye hajaridhika na huduma za mahakama, ameona dosari yoyote au ana malalamiko kuyaorodhesha ili yafanyiwe kazi.

Akizungumza na RC Malima mkoani hapa Jumatatu Mei 16, Jaji Profesa Ibrahim amesema katika fomu hiyo mwananchi atatakiwa kuandika iwapo hajaridhika na huduma aliyokusudia kuipata, hakuridhika na lugha au hajatendewa haki katika maamuzi yaliyotolewa.

"Sisi huwa tuna kawaida ya kupokea mrejesho na bahati mbaya si wananchi wengi wanafahamu kwamba anapokuwa mahakamani kupata huduma lazima aridhike ambapo kama hajaridhika anaweza kujaza fomu iwapo hajaridhika na zile huduma aidha lugha au mwenendo anaweza kujaza fomu za malalamiko sisi tutaifanyia kazi.

"Kwa hiyo nikuombe Mkuu wa Mkoa, anaweza kuja mwananchi akalalamika kwako ukamjazia hii fomu ukaiwasilisha na sisi tutaifanyia kazi.

"Fomu hii pia inapatikana kwenye mtandao lakini sasa wananchi wengi wanalalamika kwenye mtandao hawawezi kufika kwa sababu ya bundle sasa wakija kwako au wakamkuta Katibu Tawala au maofisa wako wakajaza yale malalamiko kwa niaba yako zikatumwa kwa mtandao sisi tutaziona na kuzifanyia kazi.

"Kingine sisi huwa tunafanya shughuli zetu kimkakati kwa hiyo tuna mpango wetu mkakati ukiwa mdau wa mahakama utatuambia mkoa wangu kuna mkakati fulani sisi tunakusaidia..." amesema Jaji Profesa Juma.

Kwa upande wake RC  Malima alisema Serikali ya Mkoa wa Tanga wana ushirikiano mzuri na mahakama isipokuwa changamoto kubwa ni suala la ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto.

Amesema ukatili wa kijinsia na unyanyasaji watoto unafanyika bila kificho lakini wanamalizana wenyewe ambapo hadi yeye akisikia jambo hilo anakuta  wameshafanya michezo kwenye ushahidi ambapo kesi inakuwa ngumu kuisimamia.

"Lakini hilo ni jambo ambalo linatusumbua sana na nilichogundua linawasumbua wengi kwa sababu napata malalamiko mengi sana kutoka kwa wabunge wanawake na madiwani wa viti maalumu na wawakilishi wengine wa wanawake wanakuja kulalamika kuhusu vitendo hivyo, tunaiomba mahakama ikayasimamie haya," amesema RC Malima.

Matangazo

  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA KWA SHULE ZILIZOPO MKOA WA TANGA 2021 December 21, 2020
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI -FIRST SELECTION 2022 May 14, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANAOHAMIA MSOMERA KWA HIARI SASA WAKATI WOWOTE

    June 10, 2022
  • JAJI MKUU AMKABIDHI RC MALIMA MWONGOZO KUREKEBISHA DOSARI, UTENDAJI WA MAHAKAMA TANGA

    May 19, 2022
  • Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Innocenti Bushangwa, amewataka Maafisa Habari kutimiza wajibu wao kwa kuwahabarisha watanzania jua ya kazi kubwa ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya wamu ya sita.

    May 14, 2022
  • CHUO CHA DIPLOMASIA CHATOA MADA YA ITIFAKI NA MAWASILIANO

    May 14, 2022
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.