• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

KOROGWE ‘YAJIPANGA’ KWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Imewekwa tarehe: April 12th, 2024

Watu 148,157 katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe wanatarajiwa kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji utakaofanyika baadaye mwaka huu.

Afisa Uchaguzi wa Halmashauri hiyo, Mwanaamina Mruma, amesema hayo wakati Mwenge wa Uhuru 2024 wenye ujumbe unaosema, ‘Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu’ ulipotembelea na kukagua kituo cha kupigia kura cha kata ya Kagunda, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi huo.

Mruma amesema hadi kufikia jana Jumatatu, halmashauri hiyo imefanya kazi kadhaa zikiwemo uhakiki wa maeneo ya utawala yatakayohusika kwenye uchaguzi huo, yatakayotangazwa rasmi na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kwenye Gazeti la Serikali.

Pia amesema halmashauri imehakiki vituo 610 vya kuandikishia orodha ya wapiga kura na baadaye kuwa vituo vya kupigia kura katika kata 29, vijiji 118 na vitongoji 610.

Mruma amesema hadi kufikia sasa, halmashauri hiyo ina masanduku ya kupigia kura 1,199 kati ya 2,380 na mihuri ni 118 kati ya 610 inayohitajika.

Kwa mujibu wa Mruma, halmashauri hiyo imetenga Shilingi milioni 30 kutoka mapato ya ndani kwa ajili ya uchaguzi huo, wakati Shilingi 1,077,640,296 zinatarajiwa kutoka Serikali Kuu.

Ili uchaguzi huo kuwa na ufanisi zaidi, Mruma anasema halmashauri ya wilaya ya Korogwe inatekeleza mikakati kadhaa ya kutoa elimu kwa umma kugombea na kushiriki uchaguzi huo.

Mikakati hiyo ni pamoja na kutumia mikutano wa hadhara kwenye ngazi za wilaya, tarafa nne, kata 29, vijiji 118 na vitongoji 610 vilivyopo wilayani Korogwe, kuandaa na kusambaza vipeperushi, mabango na stika za hamasa, kutumia vikundi vya nyimbo, ngoma, maigizo, mashairi, magari ya matangazo na redio.

Habari hii imeandikwa na Mashaka Mgeta wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.