• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

LISHE YAZIDI KUIMARIKA ZAIDI, UDUMAVU WAPUNGUA KWA KASI

Imewekwa tarehe: February 5th, 2025

LISHE YAZIDI KUIMARIKA TANGA, UDUMAVU WAPUNGUA KWA KASI

HALI ya lishe katika mkoa wa Tanga imeendelea kuimarika, ambapo takwimu zinaonyesha kupungua kwa kiwango cha udumavu kwa watoto chini ya miaka mitano kutoka asilimia 34 mwaka 2018 hadi 24 mwaka 2024.

Aidha, kiwango cha uzito pungufu kimepungua kutoka asilimia 15.6 hadi 11.2 katika kipindi hicho, ikiwa ni ishara kwamba juhudi za kuboresha lishe zimezaa matunda.

Akizungumza katika kikao cha tathmini ya lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2024, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, ameeleza  kuwa mafanikio haya ni matokeo ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, kuweka msukumo mkubwa kuhakikisha lishe bora inazingatiwa katika jamii, ili kupambana na utapiamlo.

Hata hivyo, Mhe Balozi Dk Batilda, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu ya lishe kwa jamii, ili kukabiliana na ongezeko la ukondefu kwa watoto, ambalo limepanda kutoka asilimia 2.7 hadi 5.6.

 Amesema, tatizo hilo linachangiwa na watoto kusumbuliwa na maradhi yanayopunguza hamu ya kula na baadhi ya wanawake kushindwa kunyonyesha watoto wao kwa usahihi.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa Tanga, Pili Mnyema, amesema Serikali imewekeza katika kuimarisha nyanja ya lishe kwa kuajiri maafisa lishe katika halmashauri zote za mkoa huo.

Amesisitiza kuwa hakuna sababu ya kushindwa kutekeleza kikamilifu afua za lishe, kwani mkoa huo una wataalamu wa kutosha kuhakikisha wananchi wanapata elimu na huduma sahihi za lishe.

Amesema, juhudi hizo zinaendelea kuboresha afya na ustawi wa watoto na jamii kwa ujumla, huku serikali ikihamasisha ushirikiano kati ya wadau mbalimbali ili kuhakikisha mafanikio zaidi katika sekta ya lishe.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.