MGUMBA AIPONGEZA COASTAL UNION, ATAKA VIPIGO VIENDELEE
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba, ameupongeza uongozi wa Coastal Union kwa timu hiyo kuichapa Mbeya City goli 1-0 na kuwataka waendeleze vichapo katika mechi zijazo za Ligi Kuu.
Akizungumza na baadhi ya viongozi wa Coastal Union leo asubuhi ofisini kwake, amewapongeza kwa ushindi huo uliopatikana mwishoni mwa wiki iliyopita katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Uwanja wa Mkwakwani na kutoa shilingi 500,000 kama mchango wake katika maandalizi ya mchezo ujao.
"Hongereni kwa ushindi. Nimefurahi sana na naomba dozi ziendelee kwenye mechi zinazofuata na natoa kiasi hiki cha fedha kama sehemu ya kuongeza nguvu katika maandalizi ya mchezo ujao," amesema Mgumba.
"Kutokana na kuwa na shughuli nyingi sikuweza kuja mchezo uliopita kama nilivyoahidi ila mechi ijayo nitakuja kuzungumza na wachezaji na nitakuwepo uwanjani," ameongeza mkuu wa mkoa.
Baada ya ushindi huo Coastal Union wanakuwa na pointi 22 na kusogea nafasi ya 13 na Jumamosi hii watakuwa Uwanja wa Mkwakwani kuikaribisha Tanzania Prisons.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.