• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MGUMBA AWAASA WALIMU

Imewekwa tarehe: February 12th, 2023






Na Emma Kigombe

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe.Omary Mgumba amekitaka Chama cha Walimu Tanzania (CWT),  kuendeleza umoja na mshikamano na kuepuka mifarakano kwa maslahi mapana ya chama hicho na walimu kwa ujumla.

Akizungumza wakati akifungua kikao cha chama hicho kilichofanyika mkoani Tanga na kujumuisha wajumbe kutoka mikoa yote nchini,  Mgumba amesema kupitia salam zao basi ni vema wakaziishi ili kudumisha umoja na mshikamano ndani ya chama ili kufikia malengo waliyojiwekea.

"Muendeleze utulivu mshikamano na umoja ndani ya chama chenu na umoja wenu kwa walimu salamu yenu hii muiishi hasa ile ya mshikamano salamu zenu zote ni nzuri ila mimi nimevutiwa na ile ukimchokoza mwalimu mmoja umewachokoza wote kwa sababu jambo la walimu ni jambo la walimu wote hivyo tuendeleze ushirikiano sababu bila kuwa na umoja hata malengo yenu hamtayafikia," alisema Mgumba.

Aidha Mgumba amesema serikali itaendelea kutoa ushirikiano siku zote kwa kuwa inatambua umuhimu wa walimu kwa Taifa.

Aidha Mgumba amemuagiza Afiisa Tawala msaidizi upande wa elimu kuhakikisha  shule za binafsi zinafuata sheria na taratibu zilizowekwa katika kuhakikisha mwanafunzi anasoma bila usumbufu wowote wa kurudishwa nyumbani sababu ya ada ama mchango wowote badala yake uongozi uwasiliane na mzazi ili kutatua changamoto hizo.

" Shule za binafsi ni kweli zina malengo katika  biashara na faida lakini serikali imetoa maelekezo mazuri juu ya suala hili lakini wenzetu wa shule binafsi mtoto kama hajalipa ada au mchango wowote adhabu ya kwanza ni kumrudisha mtoto nyumbani, huu ni ukiukwaji wa maelekezo ya serikali kama kuna mtoto hajalipa ada mtoto aendelee na masomo yake  asibugudhiwe wamiliki wa shule  na walimu wa shule hizo wawasiliane na mzazi wa huyo mtoto    Mgumb.


Aidha, Mgumba amewaomba wazazi wanaoshindwa kuwalipia ada na michango mingine watoto wao wakafanya maamuzi ya kuwahamishia watoto katika shule za serikali kwa kuwa  imewekeza fedha nyingi kwenye uboreshaji  wa miundombinu ya elimu kwa manufaa ya Watanzania wote.


"Kwa wazazi na walezi, Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  amejenga shule za kutosha ameondoa ada  zote elimu bila malipo lengo kuwawezesha  Watanzania wote watoto wao wapate elimu kwa urahisi" aliongeza Mgumba.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mgumba amewataka walimu kuendelea kufundisha elimu ya taaluma na ujuzi bila kusahau elimu ya malezi na maadili kwa watoto kwa sababu mtoto muda mwingi anakaa na mwalimu kuliko mzazi hivyo wasaidie kuwarudisha watoto  kwenye maadili mema  kwa kuzingatia mila na desturi za Kitanzania.

Mhe. Mgumba pia amewakumbusha walimu kusimamia maadili na kupinga vita vitendo vya ukatili kwa watoto kwa kuwa nao karibu na  kuwapa elimu  juu ya suala hilo. 












ReplyForward






Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA ARIDHISHWA NA WANAWAKE KUSAIDIANA, KUSEMEANA MAZURI

    May 12, 2025
  • BoT YAHIMIZA UWEKEZAJI MADUKA YA KUBADILI FEDHA TANGA

    May 09, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.