• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MGUMBA AWAFUNDA WAKUTUBI

Imewekwa tarehe: February 21st, 2023

Na Emma Kigombe


Mkuu wa Mkoa wa Tanga  Mhe. Omary Mgumba ameeleza kuwa teknolojia ndio nyenzo kubwa na muhimu katika taaluma ya ukutubi na kwa kutumia teknolojia hiyo huduma zitolewazo na maktaba zinaweza kuwafikia wateja wake popote walipo kwa urahisi.


Mgumba ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 49 wa mwaka wa  chama cha wakutubi Tanzania unaofanyika Mkoani Tanga.


“Nyenzo kubwa na muhimu katika taaluma ya ukutubi ni teknolojia ya habari na mawasiliano hivyo kwa kutumia teknolijia hiyo maktaba zinaweza kuwafikia wateja wake mahali popte walipo kwa urahisi  na ufanisi mkubwa ukilinganisha na utaratibu wa zamani wa kusubiri wateja kuja kutafuta huduma kwenye maktaba” alisema Mgumba


Aidha Mgumba amekitaka chama cha wakutubi Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa habari kuja na mwongozo wa maadili ya teknolojia ya habari na mawasiliano ambao utaweza kutumika kwenye maktaba pamoja na vituo vya habari nchini.


Alisema kuwa kutokana na maendeleo hayo ya teknolojia ya habari kwa sasa nchini na dunia kwa ujumla mwongozo huo utasaidia kutatua changamoto za kimtandao zinazojitokeza  ambazo zinachangia mmomonyoko wa maadili ya kitanzania.


Nae mwenyekiti wa chama cha wakutubi Tanzania Prof. Ally Mcharazo  alisema kuwa katika kuhakikisha maktaba zinaendana na kasi ya teknolojia wameanza kutoa mafunzo ya Tehama kwa wananchama wao na wanaamini mafunzo hayo yanaenda kuleta matokeo chanya na kuendana na madiliko ya teknolojia.


Zaidi ya wakutubi 150 wameshiriki mkutano huo wa 49 ambapo mpaka kumalizika kwake utaleta manufaa kwa washiriki wa mkutano hu na umma wote wa watanzania. 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.