Na Emma Kigombe
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Omary Mgumba ameeleza kuwa teknolojia ndio nyenzo kubwa na muhimu katika taaluma ya ukutubi na kwa kutumia teknolojia hiyo huduma zitolewazo na maktaba zinaweza kuwafikia wateja wake popote walipo kwa urahisi.
Mgumba ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 49 wa mwaka wa chama cha wakutubi Tanzania unaofanyika Mkoani Tanga.
“Nyenzo kubwa na muhimu katika taaluma ya ukutubi ni teknolojia ya habari na mawasiliano hivyo kwa kutumia teknolijia hiyo maktaba zinaweza kuwafikia wateja wake mahali popte walipo kwa urahisi na ufanisi mkubwa ukilinganisha na utaratibu wa zamani wa kusubiri wateja kuja kutafuta huduma kwenye maktaba” alisema Mgumba
Aidha Mgumba amekitaka chama cha wakutubi Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa habari kuja na mwongozo wa maadili ya teknolojia ya habari na mawasiliano ambao utaweza kutumika kwenye maktaba pamoja na vituo vya habari nchini.
Alisema kuwa kutokana na maendeleo hayo ya teknolojia ya habari kwa sasa nchini na dunia kwa ujumla mwongozo huo utasaidia kutatua changamoto za kimtandao zinazojitokeza ambazo zinachangia mmomonyoko wa maadili ya kitanzania.
Nae mwenyekiti wa chama cha wakutubi Tanzania Prof. Ally Mcharazo alisema kuwa katika kuhakikisha maktaba zinaendana na kasi ya teknolojia wameanza kutoa mafunzo ya Tehama kwa wananchama wao na wanaamini mafunzo hayo yanaenda kuleta matokeo chanya na kuendana na madiliko ya teknolojia.
Zaidi ya wakutubi 150 wameshiriki mkutano huo wa 49 ambapo mpaka kumalizika kwake utaleta manufaa kwa washiriki wa mkutano hu na umma wote wa watanzania.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.