• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

Michezo ni Afya. Watumishi wahimizwa kufanya mazoezi

Imewekwa tarehe: February 19th, 2024

Serikali Mkoani Tanga imesema itaendelea kuwaunganisha watumishi wa umma pamoja na taaasisi zilizopo mkoani humo kupitia michezo ili kujenga mahusiano na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Pili Mnyema katika bonanza la michezo Kwa watumishi wa idara na taasisi za umma mkoani Tanga.

Akizungumza Mnyema amesema michezo ni sehemu ya kuwakutanisha pamoja watumishi ambao muda mwingi wanautumia ofisini kuwatumikia wananchi.

“Undugu, ujamaa unatengenezwa baina yetu kupitia michezo kwa hiyo majumuiko kama haya ni sehemu ya kuendelea kutusogeza pamoja kama familia” alisema Mnyema.

Pia Mnyema amesema michezo ni uchumi hivyo vijana watumie fursa hiyo kujiunga na michezo mbalimbali itayowafanya wajulikane katika maeneo mbalimbali.

“Vijana wetu ambao bado mpo mashuleni tumieni fursa hii tunaona katika miaka ya hivi karibuni hatuwezi kutaja watu waliofanikiwa bila kutaja wanamichezo” aliongeza Mnyema.

Sambamba na hilo katibu tawala Mkoa wa Tanga amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka nguvu nyingi kuhakikisha michezo ndani ya taifa letu inakua na kuimarika zaidi.

Kwa upande wake afisa michezo mkoa wa Tanga Digna Tesha amesema mkoa umejipanga kuhakikisha michezo kama hiyo inafanyika kila robo ya mwaka ili kuendeleza desturi nzuri iliyoanzishwa katika kujenga uhusiano baina ya watumishi wa umma na taasisi kupitia michezo.

Kwa upande wa washiriki waliohudhuria bonanza hilo wameipongeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kwa kuandaa bonanza hilo ambalo limeleta matokeo mazuri.

Taasisi zilizoshiriki bonanza hilo la michezo ni TRA, TANESCO, GIPSA, Bodi ya Mkonge, SISALANA, Magereza,Ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoa, Jeshi la zimamoto, NMB,Bonde la maji Pangani, TAKUKURU, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo,TANGAUWASA, Uhamiaji,TPA,Vilabu vya michezo pamoja na shule mbalimbali za mkoa wa Tanga.

Imeandaliwa na Emma Kigombe, Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tanga.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.