• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWAITA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO KUKUTANA ZANZIBAR

Imewekwa tarehe: March 18th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amewaita Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki Serikalini, kushiriki Kikao Kazi cha 20 kitakachofanyika Unguja, Zanzibar kuanzia Aprili 3 hadi 6, 2025.

Wito wa Msigwa ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, umetolewa leo Machi 18, 2025 na kusambazwa na Idara ya Habari (MAELEZO), ukieleza kuwa washiriki wa Kikao Kazi wanatoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Kwa mujibu wa Msigwa, Kikao kazi hicho kinaratibiwa na MAELEZO, Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali (SMT) kwa kushirikiana na Idara ya Habari-MAELEZO (SMZ).  

Msigwa amesema wakati wa Kikao kazi hicho, kutatolewa huduma za upimaji afya na matibabu kwa washiriki, waandishi wa habari, watoto na watu wazima bila malipo.

Huduma na matibabu hayo vitatolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI).

Taarifa hiyo ya MAELEZO imeleeza, huduma za afya zitatolewa wakati wote wa kikao kazi hicho kuanzia saa 3:00 hadi 11:00 jioni kwenye uwanja wa New Amani Complex.

MAELEZO kupitia taarifa hiyo imeainisha huduma zitakazotolewa na MNH ni upimaji na uchunguzi wa figo, kisukari, macho na afya ya akili na kutoa elimu kuhusu magonjwa hayo na saratani, lishe bora na upimaji wa afya ya lishe.

Kwa upande wa JKCI itatoa huduma za uchunguzi wa kuangalia mfumo wa umeme wa moyo, shinikizo la damu, wingi wa sukari kwenye damu, kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi na uwiano baina na urefu na uzito.

Pia JKCI itatoa elimu kuhusu magonjwa ya moyo, lishe bora na matumizi sahihi ya dawa za moyo.

Nayo MOI itafanya uchunguzi wa magonjwa ya mifupa, ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu, na kuelimisha kuhusu magonjwa ya mifupa, ubongo, mgongo, mishipa ya fahamu, mazoezi tiba, ukaaji na ulalaji sahihi ili kujiepusha na maumivu ya mgongo.

“Huduma hizi ni sehemu ya huduma kwa jamii zinazotolewa kwa ushirikiano wa hospitali hizi za kitaifa na Waratibu wa Kikao Kazi cha 20 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki wa Serikali,’ imehitimisha taarifa hiyo.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.