• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MWANAMKE ATOA ENEO LAKE KWA UJENZI WA MRADI WA MAJI BUMBULI

Imewekwa tarehe: April 12th, 2024

MWANAMKE ATOA ENEO LAKE KWA UJENZI WA MRADI WA MAJI BUMBULI

MKAZI wa kijiji cha Funta katika halmashauri ya Bumbuli wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, Amina Idd, ametoa mita za mraba 17 kutoka eneo la makazi yake kwa ajili ya mradi wa maji kwa wakazi wa eneo hilo uliowekewa jiwe la msingi na Mwenge wa Uhuru 2024 jana.

Hatua hiyo imefikiwa na mkazi huyo ili kukabiliana na ukosefu wa eneo uliosababisha Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira (RUWASA) wilaya ya Lushoto, kupata changamoto ya kupata mahali panapofaa kwa ajili ya ujenzi wa tenki lenye ukubwa wa lita za ujazo 120,000, ili litumike kutoa huduma ya maji kwa wakazi zaidi ya 4,000 wa kijiji hicho na maeneo ya jirani.

Mradi huo ulifunguliwa jana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 wenye ujumbe unaosema, ‘’Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu,’’ Ndugu Godfrey Mnzava.

‘’Niliwaona RUWASA wakihangaika kutafuta eneo la kujenga mradi wao huu, waliponifuata na kutokana na kero ya maji iliyokuwepo awali, nikaona hakuna sababu ya kushindwa kutoa sehemu ya kiwanja change hiki kidogo, itume kwa mradi wa maji wenye maslahi kwa watu wengi zaidi,’’ anasema Amina.

Kwa mujibu wa Amina na uthibitisho wa uongozi wa RUWASA wilayani Lushoto, eneo hilo limetolewa bure, na kwa kutambua utayari wake huo, (Amina) aliunganishiwa huduma ya maji bure.

Faidha Adam ni mkazi wa kijiji hicho, anasema ukosefu wa maji uliwasababishia kadhia nyingi ikiwemo kuharibika kwa mahusiano kwenye ndoa, ikiwemo baadhi ya wanaume kutowaamini wake zao waliotumia muda mrefu kwenda maeneo ya mbali kutafuta maji.

Naye Angela Yusuph wa kijiji hicho anasema, ukosefu wa maji uliwasababishia kero ya kupanda milima ili kuyafikia maeneo yenye vyanzo vya maji, hukuwa wakishindwa kumudu mahitaji ya usafi wa mwili na mazingira.

Meneja wa RUWASA mkoa wa Tanga, Mhandisi Upendo Lugongo, anasema mradi huo ulioanza kujengwa Agosti 18, 2022 na kutarajiwa kukamilika kwa asilimia 100 Aprili 30 2024, umegharimu takribani Shilingi milioni 833.  

Habari hii imeandikwa na Mashaka Mgeta wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.