• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MWENGE WAELEKEZA KUDHIBITI UVAMIZI WA MAENEO YA UMMA

Imewekwa tarehe: June 14th, 2025

MWENGE WAELEKEZA KUDHIBITI UVAMIZI MAENEO YA UMMA

 

Na Mashaka Mgeta, MUHEZA 

MWENGE wa Uhuru 2025 umezielekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) kuweka na kutekeleza mipango inayolenga kudhibiti vitendo vya uvamizi wa maeneo ya umma.

Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru 2025, Ismail Ali Ussi, ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza na wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, kwenye mradi ujenzi ya Zahanati ya Kijiji cha Muungano uliopo kata ya Mlingano, uliotembelewa, kukaguliwa na kuwekewa jiwe la msingi.

Mradi huo wenye lengo la kuwezesha upatikanaji wa huduma bora za afya, kusogeza huduma za mama,baba na mtoto karibu na wananchi na hivyo kuwafanya watu kuwa wenye afya njema, unagharimu Shilingi milioni 165.9 huku walengwa wake wakiwa ni wakazi 6,258 wa kijiji cha Muungano.

Amesema kuna kasumba kwa baadhi ya maeneo ya umma na yaliyopangiwa huduma za kijamii, kuvamiwa na watu wasiokuwa na nia njema, kisha wakaachwa na kufanya maendelezo, hali inayoibua taharuki pindi wanapoondolewa.

Ussi amesema, Serikali imekuwa na mipango ya muda mfupi, kati na mrefu wa uendelezaji wa maeneo kwa shughuli za kijamii, hivyo ni muhimu kwa mamlaka za usimamizi kudhibiti aina zote za uvamizi usitokee kwenye maeneo yao

Hata hivyo,vyo, Ussi amesema watu wanaoshiriki uvamizi wa maeneo ya Serikali na yale ya umma, wanapaswa kuepuka vitendo hivyo kwani ni kinyume cha sheria zilizopo.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Dk Fani Musa akasema mradi huo unaofadhiliwa na taasisi ya Islamic Help, ukiwa umekamilika kwa asilimia 90. ulianza Machi,2, mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Agosti, 1, 2025.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

    June 18, 2025
  • RAS TANGA 'AWASHUKIA' WATUMISHI WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI

    June 18, 2025
  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.