• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MWENGE WAIFAGILIA RUWASA TANGA KUTANGAZA ZABUNI MFUMO WA MANUNUZI

Imewekwa tarehe: April 12th, 2024

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, Ndugu Mnzava ameisifu Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (RUWASA) mkoa wa Tanga, kwa kutimiza takwa la kisheria kutangaza zabuni za miradi yake kwenye mfumo wa manunuzi ya umma.

Ndugu Mnzava amesema, hatua hiyo inatoa ishara ya umuhimu wa mifumo ya manunuzi ya umma kujulikana kwa watendaji wa serikali katika ngazi zote, na kwa wajumbe wa Kamati za Usalama (KU) ili kuwa na uelewa wa pamoja katika usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya umma.

Ameyasema hayo baada ya kukagua mradi wa maji Magila Gereza, wakati Mwenge wa Uhuru 2024 wenye ujumbe unaosema, ‘Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu’ ukiwa katika siku yake ya kwanza mkoani Tanga.

Kuhusu mradi wa maji Magila Gereza, Ndugu Mnzava amesema pamoja na ubora wake, inapaswa kuongezewa nyenzo za ulinzi na usalama kwenye chanzo cha maji na tenki lililopo.

Amesema licha ya RUWASA kuendelea kutoa elimu kuhusu ulinzi shirikishi kwenye chanzo cha maji na tenki la mradi huo, jeshi la polisi kupitia kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ya Korogwe, linapaswa kuwajengea uwezo wananchi kuhusu mbinu za ulinzi kwenye chanzo cha maji na tenki lililopo.

Pia, Ndugu Mnzava amewahimiza wananchi wa Korogwe kuyalinda na kuyahifadhi mazingira ya safu ya milima ya Usambara yenye vyanzo vingi vya maji, kwa vile maji hayo ni safi, salama na yanayofaa kwa matumizi ya binadamu.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Korogwe, Mhandisi William Tupa, amesema mradi huo wenye thamani ya Shilingi 775,743,809 zilizotolewa kupitia Mfuko wa Maji (NWF), unawahudumia watu 4,543 katika vijiji vya Magila Gereza, Nkalekwa na Mgobe.

Mhandisi Tupa amesema kazi zilizopangwa na kutekelezwa kwenye mradi huo ni ujenzi wa chanzo cha maji uliofikia asilimia 95, tenki la ujazo wa lita 300,000 (asilimia 95), mtaro na kufunga mabomba mita 26,314 (asilimia 80), vilula 28 (asilimia 90) na alama za njia za bomba 264 (asilimia 20).

Habari hii imeandikwa na Mashaka Mgeta wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HISTORIA YAANDIKWA, HANDENI YAPATA CHUO CHA UUGUZI NA UKUNGA

    May 04, 2025
  • SPIKA BWZ AGAWA MITUNGI YA GESI 61 KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

    April 27, 2025
  • SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

    April 26, 2025
  • MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.