• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MWENGE WASHAURI ELIMU YA RUSHWA IJIKITE KATIKA KUZUIA

Imewekwa tarehe: April 18th, 2024

MWENGE WASHAURI ELIMU YA RUSHWA IJIKITE KATIKA KUZUIA

Na Mashaka Mgeta, KILINDI

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, Godfrey Mnzava, amehimiza elimu ya rushwa kwa jamii, hususani watoto na vijana, ijikite katika stadi za kuzuia zaidi ya kupambana na vitendo hivyo vinavyoathiri ufanisi katika utumishi wa umma na sekta binafsi.

Mnzava ameyasema hayo leo, baada ya Mwenge wa Uhuru 2024 kukagua na kuzungumza na wanachama zaidi ya 100 wa klabu ya wapinga rushwa na dawa za kulevya katika Shule ya Sekondari Mbwego iliyopo wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, kisha kuzindua klabu hiyo.

Kwa mujibu wa Mnzava, hatua hiyo itachangia kuwa na kizazi kinachopinga rushwa kwa dhamira ya dhati na mioyo iliyo wazi kuichukia, kuikataa na kuifichua (rushwa) mahali popote.

Naye Mwenyekiti wa klabu ya wapinga rushwa na dawa za kulevya katika Shule ya Sekondari Mbwego, Solomoni Isaya, amesema klabu hiyo imeanza kutumia jina hilo Machi 2024, ikitokana na klabu ya awali ya wapinga rushwa iliyoanzishwa shuleni hapo mwaka 2012 ikiwa na wanachama 42.

Solomoni ameuambia Mwenge wa Uhuru 2024 wenye ujumbe unaosema ‘’Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu’’ kuwa hivi sasa, klabu hiyo ina wanachama 162, wavulana wakiwa ni 70 na wasichana 92.

Kwa mujibu wa Solomoni, wanachama wa klabu hiyo wanapata elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na dawa za kulevya kupitia vipeperushi, majarida na masomo mbalimbali yanayotolewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Solomoni amesema, klabu hiyo inashiriki shughuli mbalimbali za uelimishaji umma kuhusu athari za rushwa na dawa za kulevya kwa nyimbo, mashairi, ngojera, uandishi wa insha, kufanya maonyesho na kuwashirikisha wazazi, walezi na wanafunzi wenzao kuhusu madhara ya rushwa.

Kwa upande mwingine, Mwenge wa Uhuru 2024 ulikagua na kuridhishwa na uendelevu wa miradi iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru 2023, kuzindua darasa moja lililopo katika Shule ya Sekondari Mbwego lililogharimu Shilingi milioni 20  zilizotolewa na Serikali Kuu huku nguvu za wananchi zikiwa ni Shilingi 700,000.

Ukiwa katika wilaya ya Kilindi, Mwenge wa Uhuru 2024 umepanda miti na kuifikia miradi nane ya maendeleo kwa kuitembelea, kukagua uendelevu, kuweka jiwe la msingi na uzinduzi,

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.