• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

PROFESA KABUDI AIBUA HISTORIA YA ZANZIBAR AKITOA ASILI YA JINA BUBUBU

Imewekwa tarehe: April 8th, 2025


Na Mashaka Mgeta, ZANZIBAR

WAPO wanaomtambua kwa ufasaha wa lugha hasa Kiswahili, wengine wanamjua zaidi kwa umahiri wa imani na mapokeo ya dini, sasa amedhihirisha sehemu ndogo ya namna anavyoielewa Zanzibar.

Huyo si mwingine, bali ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe Profesa Paramagamba Kabudi, aliyefika Zanzibar kwa mara ya kwanza mwaka 1978, akiwa Mwandishi wa Habari. Imefika takribani miaka 47.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe Hemed Suleiman Abdulla, kufungua Kikao Kazi cha 20 cha Maafisa Mawasiliano, Habari, Uhusiano na Itifaki Aprili 3, 2025 mjini Unguja, Mhe Profesa Kabudi, akaeleza anavyoifahamu historia ya Zanzibar iliyo sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe Abdulla alifungua Kikao Kazi hicho kwa niaba ya Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Mhe Profesa Kabudi akasema, kwa kipindi chote hicho, hakujawahi kuwepo kasi kubwa ya maendeleo, ikiwemo miundombinu na ustawi wa watu wa Zanzibar kama sasa, chini ya uongozi wa Mhe Dkt Mwinyi.

Akatoa mfano kuwa, miongoni mwa viashiria vya ukuaji maendeleo ya Zanzibar ni miundombinu inayofungamana na kuchochea shughuli na ukuaji wa uchumi.

Hapo, akaibua historia ya reli iliyokuwepo awali, ikitoa huduma za usafiri na usafirishaji kutoka maeneo ya katikati ya Unguja kwenda Bububu, jina lenye asili inayotokana na kelele za ‘bu-bu-bu…’ zilizotoka kwenye treni iliyotumia reli hiyo.

Historia hiyo ikamvutia Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Zanzibar, Tabia Maulidi Mwita ambaye - kwa mujibu wa Mhe Abdulla, alionesha kushangazwa na ufahamu wa Mhe Profesa Kabudi kuhusu historia ya Zanzibar.

Akifungua Kikao Kazi hicho, Mhe Abdulla, pamoja na mambo mengine, akagusia hoja ya Mhe Profesa Kabudi kuhusu Bububu, akasema hivi sasa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ipo kwenye mchakato wa kujenga reli hiyo, itoe huduma bora na za kisasa.

Mhe Abdulla akasema, utaratibu wa mchakato huo umeshaanza, kisha akathibitisha kwa Mhe Profesa Kabudi kuwa ‘ndoto yake’ kuhusu kurejea kwa reli hiyo itatimia inshallah.

Naye Mhe Mwita akamtaja Mhe Profesa Kabudi kama ‘maktaba inayotembea’, na kwamba ushirikiano wa wizara wanazoziongoza, uliowezesha kufanyika kwa Kikao Kazi cha 20 huko Unguja ni ishara ya kuzidi kuimarika kwa Muungano.

Mhe Mwita akasema Kikao Kazi hicho kimewaweza washiriki kuyaona maendeleo yalifikiwa Zanzibar, kushiriki utalii wa ndani, kuendeleza na kudumisha ushirikiano wa kabla na baada ya Muungano wa Aprili 26, 1964.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.