• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC BATILDA AZINDUA KAMPENI YA CHANGO YA MIFUGO, ATOA WITO KWA WAFUGAJI

Imewekwa tarehe: August 21st, 2025

Na Emma Kigombe, OMM TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Dkt. Batilda Burian, amezindua  Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya Mifugo katika viwanja vya Chuo cha Mafunzo ya Mifugo (LITA – Buhuri) jana Agosti 20, 2025.

Mhe Balozi Dkt Batilda  amesema Tanga imejipanga kuchanja zaidi ya mifugo milioni mbili ili kudhibiti magonjwa na kuongeza tija katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya wananchi na uchumi wa taifa.

Amesema, kampeni hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kulinda na kuendeleza rasilimali za mifugo, uliozinduliwa na Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,  Juni 16, 2025 mkoani Simiyu. 

Alisisitiza kuwa chanjo ya mifugo ni nyenzo muhimu katika usalama wa chakula, ustawi wa jamii, afya ya binadamu  na utunzaji wa mazingira.Mhe Balozi  Dkt. Batilda amesema kuwa kwa Mkoa wa Tanga pekee, kampeni hiyo inalenga kuchanja ng’ombe 668,000 , mbuzi na kondoo 1,055,700 na kuku 1,162,200 hatua ambayo inalenga kuimarisha afya ya mifugo, na kuzuia milipuko ya magonjwa ambayo huathiri uzalishaji na maisha ya wananchi wengi wanaotegemea sekta hiyo kwa kipato. 

Aidha, alieleza kuwa mkoa huo umepokea vifaa muhimu vya kutekeleza kampeni hiyo, ikiwa ni pamoja na dozi za chanjo, vishikwambi, barafu za kuhifadhia chanjo, sindano, hereni za mifugo na mavazi ya kujikinga kwa wataalamu wa afya ya mifugo.Katika hatua nyingine, Mge Balozi Dkt. Batilda ametoa wito kwa wafugaji kuhakikisha mifugo yao inafikishwa katika vituo vya chanjo, vilivyopangwa katika maeneo yao ili kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa kwa asilimia 100.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DC MKINGA: TUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA KUZUIA UBAKAJI, UKATILI

    August 27, 2025
  • HALMASHAURI 34 ZAAGIZWA KUWAPELEKA WANAMICHEZO SHIMISEMITA

    August 23, 2025
  • RC BATILDA: TUMEWAFUNDISHA, MTENDEENI HAKI MAMA SAMIA

    August 23, 2025
  • WAZIRI JAFO: SERIKALI KUJENGA VIWANDA VIPYA 9,048

    August 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.