• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC Kindamba amaliza mgororo wa miaka 17

Imewekwa tarehe: September 16th, 2023

Na Mashaka Mgeta, Kilindi

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Waziri Kindamba ametumia dakika 17 kumaliza mgogoro uliodumu kwa miaka 17 ukihusisha mpaka kati ya vijiji vya Gitu na Ngobole Wilayani Kilindi.

Hatua hiyo imefikiwa na Mhe. Kindamba aliyefuatana na Kamati ya Usalama (KU) ya Mkoa wa Tanga na Katibu Tawala Mkoa, Pili Mnyema.

Mgogoro huo ulihusu mpaka wa kijiji cha Gitu na Ngobole ambapo vitongoji vilivyokuwa na mgogoro ni Komtindi na Ng'aloji ambavyo vimesajiliwa kijiji cha Gitu, ila mpaka wa ramani ya upimaji wa vijiji hivyo ulipoainishwa ardhini ilibainika vitongoji hivyo kuwa katika Kijiji cha Ngobole.

Akionekana kukerwa na mgogoro huo uliotajwa pia na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokutana hivi karibuni na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Mkoa, Mhe. Kindamba akasema, kwa mujibu wa tamko rasmi la Serikali (GN), vitongoji hivyo vipo katika kijiji cha Gitu.

Ameuagiza uongozi wa Gitu na Ngobole kuandaa muhtasari wa mkutano aliotoa agizo hili ili kuweka kumbukumbu kwenye mamlaka husika.

Mhe. Kindamba amesema haiwezekani kwa mkoa wa Tanga unaopokea fedha nyingi za miradi ya maendeleo kutoka kwa Mhe. Dk Samia, ushindwe kujikita kwenye maendeleo ya ustawi wa wananchi, badala yake ubaki kushughulikia migogoro isiyokuwa na tija kama wa mpaka unaotambuliwa na GN.

Mhe. Kindamba ameiagiza halmashauri ya Wlĺ4ilaya ya Kilindi, kwa usimamizi wa Mkuu wa Wilaya hiyo, kuweka alama za kudumu za kutenganisha maeneo ya vijiji hivyo.

Pia, Mhe. Kindamba amesema eneo la takribani hekta 2000 lililopo kwenye eneo hilo limekabidhiwa kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ili walitumie kwa mazoezi ya ulinzi na usalama.

Amesema JWTZ iliwahi kuliomba eneo hilo muda mrefu, lakini ombi lao bado halijashughulikiwa.

Mhe. Kindamba akatumia fursa hiyo kuwaonya viongozi wa vijiji hususani wenyeviti wilayani Kilindi na kwingineko mkoani Tanga, kuacha kujihusisha na uuzaji holela ya maeneo ya vijiji vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

"Viongozi tunapaswa kuwatumikia wananchi badala ya kujinufaisha binafsi, tufuate Sheria, Kanuni na Taratibu...hali ya Kilindi katika maeneo hayo haipo vizuri," ameonya.

Mhe. Kindamba akawataka wananchi wa Kilindi kuepuka migogoro ya ardhi inayowafikisha kupigana na kupeana majeraha.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.