• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

RC TANGA AWATAKA WATUMISHI WASISABABISHE KADHIA KWA WANANCHI

Imewekwa tarehe: January 29th, 2026

Na Mashaka Mgeta, SAADANI


MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt. Batilda Burian, amewataka watumishi wa umma mkoani humo, kujiepusha na vitendo vinavyoashiria ama kusababisha kadhia kwa wananchi wanaofika kupata huduma kwenye maeneo yao.

Mhe Balozi Dkt Batilda, ameyasema hayo wakati akifunga kikao cha Baraza la Wafanyakazi mkoani Tanga, kilichofanyika jana Januari 27, 2026 kwenye Hifadhi ya Taifa ya Saadani.

Amesema, pamoja na mwenendo mzuri wa kujivunia kwa utumishi wa umma kwa utoaji huduma wenye kuridhisha mkoani humo, ipo haja ya kuendeleza utendaji kazi unaojali utu, weledi na maadili katika hatua zote zinazohusiana na utendaji kazi wao.

“Tuyatekeleze haya mahali popote tunapotoa huduma, kama ni ofisini basi iwe tangu mwananchi anapoingia getini, anavyopokewa, lugha na matendo yetu visiwe vyenye kusababisha kadhia kwao,” amesema.

Pia, Mhe Balozi Dkt. Batilda amewahimiza watumishi katika Sekretarieti ya Mkoa (RS) kuimarisha zaidi mifumo na ufuatiliaji wa miradi na huduma zinazotolewa na Serikali, ili kukidhi thamani ya fedha zinazotolewa.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, alisem a wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi, walijadili kwa kina, uhuru na uwazi masuala yanayowahusu katika kufikia malengo ya Serikali kuwatumikia wananchi.

Alisema, watumishi wa umma kutoka idara na vitengo vyote wamethibitisha kutambua na nafasi na umuhimu wa majukumu yao, hivyo kuahidi kuendelea kuwajibika kadri ya maadili ya utumishi wa umma.


Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA 'AWAFUNDA' WATUMISHI TANGA AKIHIMIZA UFANISI, TIJA

    January 29, 2026
  • RC TANGA AWATAKA WATUMISHI WASISABABISHE KADHIA KWA WANANCHI

    January 29, 2026
  • AWESO AKABIDHI VIFAA VYA MRADI WA MAJI MKINGA-HOROHORO

    January 17, 2026
  • VIJANA PANGANI 'WAKOSHWA' NA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    November 27, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.