• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TANGA TUNA UTOSHELEZI WA CHAKULA - BALOZI BATILDA

Imewekwa tarehe: July 17th, 2025

Na Mashaka Mgeta, DODOMA

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amethibitisha kuwepo utoshelezi wa chakula mkoani humo, unaotokana na maboresho ya sekta ya kilimo yaliyofikiwa katika Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Mhe Balozi Dkt Batilda ameyasema hayo juzi Julai 15, 2025, alipokuwa akizungumza kwenye Mkutano wa Waandishi wa Habari ulioandaliwa na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali jijini Dodoma.

Amesema, katika kipindi cha takribani miaka minne ya uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia, Tanga imepokea Shilingi bilioni 33.3 kwa shughuli za kilimo.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema, miongoni mwa mafanikio yaliyotokana na uwekezaji huo ni kutolewa kwa pembejeo za ruzuku kama vile mbegu bora na mbolea kwa wakulima 134,527 waliosajiliwa kidigitali. 

Wakulima 11,198 walinufaika na tani 4,235.35 za pembejeo kwa gharama ya Shilingi bilioni 8.1 huku ruzuku ya Serikali ikiwa ni Shilingi bilioni 2.5.

Pia, amesema pikipiki 380 zenye thamani ya Shilingi milioni 950, vishikwambi 371 vya ukusanyaji takwimu (Shilingi milioni 296.8) na vipima odongo saba (Shilingi milioni 153) kwa upimaji na ushauri wa kitaalamu kwa wakulima vimetolewa mkoani humo hivyo kuongeza ubora na wingi wa uzalishaji mazao.

“Hali ya chakula mkoani Tanga na nzuri na toshelezi,” amesema na kutoa mfano kuwa, msimu wa 2023/24, kilimo kilifanyika kwenye jumla ya hekta 909,076 za mazao ya chakula, na kuzalisha tani 2,659,802 (ghafi), sawa na tani 1,314,292.4 za chakula kikavu. “Uzalishaji huu umetosheleza mahitaji ya wakazi wapatao 2,615,597 wa mkoa huu, na kuwa na ziada ya chakula kwa ajili ya biashara na hifadhi,” amesema. 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAANDISHI DODOMA WAVUTIWA NA MAENDELEO YA TANGA, WAALIKWA KUFANYA ZIARA

    July 17, 2025
  • RC BATILDA:ONGEZEKO LA WATU TANGA ISHARA YA UBORA WA HUDUMA ZA FYA, USTAWI WA JAMII

    July 17, 2025
  • TANGA TUNA UTOSHELEZI WA CHAKULA - BALOZI BATILDA

    July 17, 2025
  • BALOZI BATILDA ASEMA TANGA INA HIFADHI YA LITA ZA UJAZO MILIONI 210 ZA MAFUTA

    July 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.