• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TANGA YATANGAZA MPANGO WA KUMUENZI SHAABAN ROBERT

Imewekwa tarehe: January 1st, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

HATIMAYE mkoa wa Tanga umetangaza mpango wa kumuenzi nguli za fasihi, ndani na nje ya nchi, marehemu Shaaban Robert aliyezaliwa Januari Mosi, 1909 na kufariki dunia Juni 22, 1962.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, ameyasema hayo kwenye kongamano la kukumbuka kuzaliwa kwa Shaaban Robert, lililofanyika leo Januari 1, 2025 kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Kongamano hilo limewajumuisha wazee, wakiwamo wenye simulizi za maisha na falsafa ya Shaaban Robert, watumishi wa umma, wajasiriamali na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pongwe walioghani mashairi mbalimbali yenye maudhui yanayofanana na malengo ya kongamano hilo.

Mhe Balozi Dk Batilda amesema sehemu ya mpango huo, inahusisha kuanzisha Shindano la Shaaban Robert kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, kisha kutoa zawadi kwa washindi ili kuchochea ari ya kuandika na kusoma vitabu, riwaya, mashairi na kuziishi falsasa za Shaaban Robert.

Amesema, mpango huo utahusisha pia kuendeleza kongamano hilo kila mwaka, kutafuta na kuhifadhi kwenye maktaba ya mkoa, nakala za vitabu, mashairi na maandishi mengine yaliyopo, vinavyotambulisha kazi za Shaaban Robert. 

Mtafiti wa lugha, Bakari Nauma, amesoma wasifu wa marehemu Shaban Robert ‘uliogusia’, malezi katika familia, elimu na maeneo tofauti aliyofanya kazi ikiwemo idara ya forodha Pangani, alipokuza kipawa cha fasihi andishi, idara ya wanyamapori Mpwapwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tanga.

Mwalimu Musa Mayombe  wa Shule ya Msingi Pongwe, anasema wapo wanafunzi wanaoshiriki nyanja mbalimbali zinazothibitisha kuwa na vipawa tofauti ikiwa ni pamoja na ushairi, hivyo ipo haja ya mpango kuwatambua na kuendeleza vipawa hivyo.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.