• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TASAF TANGA YAWAGUSA WABUNGE,WATAKA VIONGOZI BORA KUTETEWA,KULINDWA

Imewekwa tarehe: March 14th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

UTEKELEZAJI wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF)-awamu ya tatu mkoani Tanga, umewaridhisha wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria waliopo kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo.

Taarifa ya TASAF iliyosomwa na Katibu Tawala Mkoa (RAS), Pili Mnyema, imeeleza takribani Shilingi bilioni 15 zimetolewa na Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa uhawilishaji kwa walengwa 68,906.

Mnyema alisema, kupitia utekelezaji wa miradi ya ajira za muda (PWP), Tanga imeibua miradi 750 kati ya 825 (sawa na asilimia 91) ya kutoa ajira za muda kwa walengwa wa TASAF.

Kwa mujibu wa Mnyema,  miradi hiyo ilihusu ukarabati wa barabara za vumbi, vivuko vya waenda kwa miguu, bwawa na banio la umwagiliaji, vyanzo vya maji, miti ya mbao na upandaji miti ya matunda.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe Dkt Joseph Mhagama, amesema ufanisi wa miradi ya TASAF mkoani Tanga ni matokeo ya utashi wa kisiasa wa Mhe Rais Dk Samia, na usimamizi shirikishi wa viongozi mkoani humo.

Amesema mnyororo huo wa uongozi chini ya Mhe Rais Dkt Samia, unadhihirisha uwepo wa viongozi bora nchini na ambao, kimsingi, wanapaswa kutetewa na kulindwa wakati wote.

Mhe Dkt Mhagama, alitoa mfano wa viongozi hao kuwa ni Mkuu wa Mkoa, Mhe Dkt Batilda Burian, Katibu Tawala Mkoa, Pili Mnyema na wabunge wa  majimbo na kuteuliwa wa mkoa huo, akiwemo Mhe Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo na mjumbe wa kamati hiyo.

Mhe Balozi Dkt Batilda alisema, Pamoja na TASAF, Tanga imepokea takribani Shilingi trilioni 3.1 kwa ajili ya miradi ya kisekta kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia.

Amesema, fedha hizo zimetumika kwa miradi ya maendeleo na ustawi wa jamii, pamoja na majengo ya utawala kwa halmashauri zikiwemo Bumbuli na Handeni Mji zilizozinduliwa na Mhe Rais Dkt Samia hivi karibuni.   

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • RC BATILDA ATAKA MAADILI, UTAWALA BORA KUIMARISHWA SERIKALINI

    June 25, 2025
  • MIAKA MINNE, SIKU 23 ZA RAS MNYEMA TANGA, AHAMISHIWA PWANI

    June 24, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.