• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

UCHAGUZI MKUU 2025 KUING'ARISHA ZAIDI TANZANIA KIMATAIFA

Imewekwa tarehe: February 2nd, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

MOJA ya vigezo vinavyoitambulisha nchi kuwa na kiwango cha juu cha demokrasia ya kweli, ni mfumo wa Uchaguzi Mkuu ulio huru, wazi na haki, unaotoa fursa pana ya ushiriki wa wadau katika hatua zote za mchakato wake.

Ndivyo inavyodhihirika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2025 ambapo hivi sasa, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) inaboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye mikoa ya Tanga na Pwani.

Mwenyekiti wa INEC, Jaji wa Rufaa, Jacobs Mwambegele, anafungua mafunzo ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoani Tanga leo Februari 2, 2025, yanayowashirikisha Mratibu wa Uandikishaji Mkoa, Maafisa Uandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri.

Anasema, Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utakidhi vigezo ambavyo (kwa mujibu wa misingi ya uchaguzi huru na haki) vitaing’arisha nchi kimataifa, ikiwemo kuwaruhusu waangalizi wa nje na ndani ya nchi kushiriki kwa upana zaidi.

Jaji Mwambegele anasema taasisi 42 za waangalizi wa ndani na nje ya nchi, zimethibitishwa kushiriki uangalizi wa uchaguzi huo, ambapo kati ya hizo, tisa ni za kimataifa na 33 za kitanzania.

Kwa mujibu wa Jaji Mwambegele, taasisi hizo zinapaswa kupewa ushirikiano katika ngazi ili zitimize wajibu na majukumu yao ipasavyo, yatakayoudhihirishia ulimwengu ukweli kuhusu ubora wa uchaguzi wa Tanzania utavyofanyika kwa misingi ya uhuru, haki, amani na uwazi.

Mbali na waangalizi hao, Jaji Mwambegele amesema fursa nyingine inayodhihirisha utayari wa Serikali ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, kufanya uchaguzi huru na haki ni ushiriki wa taasisi za kiraia 157 zitakazotoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kushiriki uchaguzi huo wenye kauli mbiu inayosema, ‘’Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora’.

UTUNZAJI VIFAA VYA UANDIKISHAJI

Jaji Mwambegele amewaagiza maafisa wanaohusika na uchaguzi kuvitunza vifaa vya uboreshaji na uandikishaji wapiga kura, kwa vile vimegharimu fedha nyingi na vinahitajika kwenye maeneo mengine.

Amesema, kutokuwa makini katika utunzani wa vifaa hivyo, kutaathiri mwenendo wa uboreshaji na uandikishaji wapiga kura kwenye mikoa, wilaya na halmashauri ambazo hazijafikiwa na huduma hiyo.

INEC inatarajia kuandikisha wapiga kura 244,805 mkoani Tanga ikiwa ni sawa na asilimia 18.7 ya wapiga kura 1,304,235 waliopo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, na hivyo kufanya idadi yake kufikia 1,549,040.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC TANGA AMKABIDHI GARI MPYA MKUU WA WILAYA YA HANDENI

    July 12, 2025
  • RAS TANGA ASISITIZA UWEKEZAJI KWENYE MALEZI, MAKUZI YA MTOTO

    July 09, 2025
  • PINDA AHIMIZA USHIRIKIANO ENDELEVU WA SERIKALI, WANANCHI

    July 09, 2025
  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.