• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

VIJANA WATAKIWA KUWA WABUNIFU KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA AJIRA

Imewekwa tarehe: November 28th, 2024

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

VIJANA wametakiwa kutumia stadi bunifu zinazojikita katika misingi ya kizalendo kwa taifa, ili kuibua shughuli, miradi ama huduma zitakazowawezesha kupata kipato, na hivyo kuondokana na athari zinazotokana na ukosefu wa ajira.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian, ameyasema hayo leo Novemba 25, 2024, alipozungumza na Balozi wa Mazingira na Uhamasishaji, Michael Msechu aliyefika ofisi kwake kumuaga, baada ya kuhitimisha ziara kwenye wilaya nane za mkoa huo.

Amempongeza Msechu kwa kujitolea kwake kuhamasisha umma kuhusu umuhimu wa hifadhi ya mazingira, kazi inayomfikisha kwenye maeneo tofauti ya nchi, akiielimisha na kuihamasisha jamii kuhusu umuhimu na faida za hifadhi ya mazingira.

Mhe Balozi Dk Batilda amesema haistahili kwa vijana kusubiri mafanikio yasiyotokana na jitihada zao, hivyo ubunifu na kujituma vinapaswa kuwa nyenzo za kuwaongoza katika kufikia malengo yao.

Naye Msechu amesema pamoja na elimu na hamasa kuhusu hifadhi ya mazingira, amezungumza na vijana na kuwashirikisha namna tofauti za kujiendeleza na kulitumikia taifa.

Pia amesema amekutana na wananchi walioelezea kuridhishwa na namna Serikali ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, inavyotekeleza ahadi zake kwa kuanzisha na kuendeleza miradi katika sekta mbalimbali zinazogusa maendeleo na ustawi wa watu.  

Vijana walioteuliwa kuunda timu za kuendeleza ari ya hifadhi ya mazingira kutoka wilaya za mkoani humo, wamesema ziara ya Msechu imekuwa yenye manufaa kwao.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BALOZI BATILDA AHIMIZA UMOJA, MSHIKAMANO TANGA

    June 18, 2025
  • RAS TANGA 'AWASHUKIA' WATUMISHI WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI

    June 18, 2025
  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.