• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

WABUNGE WASHANGAZWA UKUAJI WA BANDARI YA TANGA...'WAMPA TANO' RAIS SAMIA

Imewekwa tarehe: March 13th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeelezea kustaajabishwa na kasi kubwa ya maendeleo kwenye bandari ya Tanga, iliyoboreshwa kwa gharama za Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe Selemani Kakoso, amesema aliposhiriki ziara ya Mhe Rais Dkt Samia bandarini hapo Machi Mosi, 2025, alishuhudia ‘mabadiliko makubwa’, ikilinganishwa na miaka mitatu iliyopita.

Kwa mujibu wa Mhe Kakoso, Kamati hiyo ilifanya ziara bandarini hapo mwaka 2023 na kubaini umuhimu wa kuwepo maboresho, ili ichangie ufanisi katika mpango wa kuifanya Tanga kuwa Mkoa wa ki-mkakati katika masuala ya uchumi na biashara.

Mhe Kakoso anasema katika kipindi hicho, Kamati yake ilibaini ucheleweshwaji wa malipo kwa maboresho ya bandari hiyo, hivyo kuishauri Serikali itoe fedha zilizoidhinishwa na Bunge kwa ajili hiyo.

Hata hivyo, Mhe Kakoso, licha ya kutotaja kiasi cha fedha walichotarajia, anasema Shilingi bilioni 429.1 zilizotolewa kwa wakati mmoja zilikuwa nyingi, na hivyo kudhihirisha utashi wa Mhe Rais Dkt Samia katika kufanikisha maboresho ya bandari hiyo.

“Nilitembelea bandari hiyo na kamati hii mwaka 2023, tukaikuta katika hali duni na miundombinu isiyokidhi ufanisi na ushindani kwenye soko, lakini fedha nyingi zilizotolewa na Mhe Rais Dkt Samia zimefanya maboresho na kuleta maendeleo makubwa sana,” amesema.

Amesema, Serikali inapaswa kushughulikia miundombinu wezeshi itakayochochea ufanisi wa huduma za bandarini ikiwemo reli na  ujenzi wa barabara ya Handeni - Kibirashi - Kiteto – Nchemba - Singida yenye urefu wa kilomita 460 na ile ya Tanga - Pangani - Saadan – Makurunge (kilomita .

Hata hivyo, akiwa katika ziara yake mkoani humu, Mhe Rais Dkt Samia, aliiagiza Wizara ya Miundombinu kushirikiana na wadau wengine ikiwemo sekta binafasi ili kugharamia ujenzi wa barabara ya Handeni - Kibirashi - Kiteto - Nchemba – Singida yenye kilomita 460.

UMUHIMU WA ZIARA ZA WABUNGE

Mhe Kakoso anasema ziara zinazofanywa na Kamati za Bunge zina manufaa makubwa, ikiwemo ‘kuisukuma’ Serikali kukamilisha miradi hasa inayokwamishwa kutokana na ukosefu wa fedha.

Amesema ziara hizo zinatajwa kwenye Kanuni za Bunge na hivyo kuzihalalisha hasa kipindi hiki cha kuelekea kwenye bajeti ya mwaka mpya wa fedha 2025/2026.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SARUJI TANGA YAKABIDHI BAJAJI ZA UMEME 10 KWA BALOZI BATILDA

    July 03, 2025
  • RC TANGA ASULUHISHA MGOGORO WA ARDHI TAFSIRI HASI YA RAMANI IKITAJWA CHANZO

    July 03, 2025
  • RAS MCHATTA: SINA MANENO MENGI, NIPIMENI KWA KAZI, UWAJIBIKAJI

    June 30, 2025
  • BALOZI BATILDA AAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO, AWAAPISHI WAWILI TANGA

    June 30, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.