Serikali mkoani Tanga imeagiza Watumishi wa Umma 20 kusimamishwa kazi na kukamatwa na Polisi pamoja na wafanyabiashara 3 kukamatwa na Polisi kupisha uchunguzi katika sakata la vitenge kuungua kwenye ghala la Mamlaka ya Mapato Bandarini Tanga Octoba mwaka huu.
Watumishi wa Umma hao ni wa Mamlaka ya Mapato (TRA) (7), Mamlaka ya usimamizi wa bandari (TPA) (6), wafanyakazi wa Suma JKT (7), na wafanyabiashara(3) wa vitenge na samaki.
Agizo hilo amelitoa leo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omary Mgumba baada ya kupokea taarifa ya Kamati ya watu 10 iliyoongozwa na Mwenyekiti Sebastian Masanja ya uchunguzi wa tukio la moto uliotokea Oktoba 23 mwaka huu na kuteketeza ghala la TRA lililokuwa limehifadhi mali za magendo zilizomatwa Wilayani Mkinga
"Uchunguzi wa kamati yangu umebaini kuwa tukio la moto ulioteketeza ghala hilo ni hujuma hivyo lazima hatua za nidhamu na za kisheria zichukuliwe" alisisitiza Mkuu huyo
Awali akiwasilisha taarifa ya uchunguzi Mwenyekiti wa Kamati hiyo Sebastian Masanja amesema kutokana na hadidu rejea walitakiwa kufualia kama moto huo lilikuwa hujuma, ajali au bahati mbaya au ugaidi ambapo imeonekana tukio zima lilikuwa ni hujuma.
"Mawasiliano hayo ya simu za watuhumiwa, nyaraka, picha za mnato na maelezo ya wahojiwa yote yalepelekea kubaini kuwa ni kitendo cha hujuma" alifafanua zaidi.
Amesema uchunguzi umebaini moto huo haukuwa ni hitilafu ya umeme na hivyo imejiridhisha kuwa moto haukuwa ni hitilafu ya umeme kwa sababu siku hiyo haukukatika na zilikuwa voti 6.6 ya umeme hata Mamlaka ya hali ya hewa inasema hakukuwa na mgandamizo wa bidhaa na nyuzi joto ilikuwa ya kawaida tu" amesema Masanja.
Golf Area/Masiwani Road Tanga
Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga
Simu: 027 2642421
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz
Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.